Mfalme wa Ryhmes, Afande Sele amesindikizwa na mamia ya
wakazi wa mkoa wa Morogoro pamoja na baadhi ya wasanii wenzake akiwemo
Joseph Haule ”Prof Jay” na Rais wa Shirikisho la Filamu, Simon
Mwakifwamba kwenye mazishi ya mama watoto wake aliyezikwa kwenye
makaburi ya Kolla mkoani Morogoro. Tazama Picha za mazishi hapo chini..
Sheikh akisoma dua kwa ajili ya marehemu mama Tunda kabla ya kwenda kumpumzisha kwenye makazi yake ya milele
Rais wa Shirikisho la Filamu TAF, Simon Mwakifwamba akimfariji Afande Sele
Afande Sele akiwa amembeba mtoto wake wa pili Asantesana
Afande Sele alkilia kwa uchungu wakati wakielekea kwenye kumzika mama watoto wake pembeni yake ni Professor Jay
Afande Sele akiweka udongo kwenye kaburi la Mama Tunda
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amen.
0 comments:
Post a Comment